Menu
NDOTO ZANGU
  • ORODHA YA NDOTO
  • MASOMO YA WANAWAKE
  • QUIZZES/ MITIHANI YA BIBLIA
NDOTO ZANGU

SIFA NI ZAKO BWANA

Posted on December 26, 2022

Zaburi 65:4-13

[4]Heri mtu yule umchaguaye,
Na kumkaribisha akae nyuani mwako.
Na tushibe wema wa nyumba yako,
Patakatifu pa hekalu lako.

[5]Kwa mambo ya kutisha utatujibu,
Katika haki, Ee Mungu wa wokovu wetu.
Wewe uliye tumaini la miisho yote ya dunia,
Na la bahari iliyo mbali sana,

[6]Milima waiweka imara kwa nguvu zako,
Huku ukijifunga uweza kama mshipi.

[7]Wautuliza uvumi wa bahari,
Uvumi wa mawimbi yake,
Na ghasia ya mataifa;

[8]Kwa hiyo wakaao mbali kabisa huogopa ishara zako; Milango ya asubuhi na jioni waifurahisha.

[9]Umeijilia nchi na kuisitawisha,
Umeitajirisha sana;
Mto wa Mungu umejaa maji;
Wawaruzuku watu nafaka
Maana ndiwe uitengenezaye ardhi.

[10]Matuta yake wayajaza maji;
Wapasawazisha palipoinuka,
Wailainisha nchi kwa manyunyu;
Waibariki mimea yake.

[11]Umeuvika mwaka taji ya wema wako;
Mapito yako yadondoza unono.

[12]Huyadondokea malisho ya nyikani,
Na vilima vyajifunga furaha.

[13]Na malisho yamevikwa kondoo,
Na mabonde yamepambwa nafaka,
Yanashangilia, naam, yanaimba.

PDF
Subscribe
Login
Notify of
guest

guest

0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments

Recent Comments

  1. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI, INJILI YA MATHAYO
  2. Noel Swai on MASWALI, INJILI YA MATHAYO
  3. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI YA KITABU CHA YOSHUA I
  4. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI YA KITABU CHA MWANZO
  5. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI YA KITABU CHA MWANZO

Palipo na Roho wa Bwana hapo ndipo penye uhuru
©2025 NDOTO ZANGU | Powered by SuperbThemes & WordPress
wpDiscuz