Menu
NDOTO ZANGU
  • ORODHA YA NDOTO
  • MASOMO YA WANAWAKE
  • QUIZZES/ MITIHANI YA BIBLIA
NDOTO ZANGU

KUOTA UPO JANGWANI PEKE YAKO

Posted on October 12, 2022October 22, 2022

Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo litukuzwe milele…….

Karibu upate kujifunza kwa njia ya ndoto.

Asilimia kubwa ya ndoto tunazoota huwa zinatokana na shughuli nyingi tunazokutana nazo…mara  nyingi ule mfumo unakuwa unajijirudia kwa njia ya ndoto…

Lakini kama umeona ndoto uliyoiota imekuja kwa uzito kidogo  na haijaja kulingana na mizunguko yako mingi.. basi yakupasa uitafari kwa kutafuta maana yake mana hapo kuna jambo Bwana anatamani ulifahamu..

Biblia inasema..

Mhubiri 5:3
[3]Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.

Hivyo basi ukiota upo Jangwani peke yako au umeota upo katika jangwa mwenyewe na hakuna msaada wowote… ni ishara Yesu anakuonyesha jinsi gani ulivyomwacha Bwana na kuliweka tegemeo lako kwa vitu vya ulimwengu huu…yawezekawa ni wanadamu, mali, au wazazi….

Maandiko yanasema…

Yeremia 17:5-6
[5]BWANA asema hivi,
Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu,
Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake
Na moyoni mwake amemwacha BWANA.

[6]Maana atakuwa kama fukara nyikani,
Hataona yatakapotokea mema;
Bali atakaa jangwani palipo ukame,
Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Jichunguze ni wapi umeweka tegemeo lako, jiangalie ni wapi umeweka tegemeo la  maisha yako kwa wanadamu, wapi umeliweka tumaini lako mpaka umemsahau na kumwacha Bwana……

Jirekebishe na ugeuke kwa kutubu na kumrudia Bwana Yesu,awe mwokozi na tegemeo la maisha yako milele….

 

Bwana wetu anakuja…..



 

PDF
Subscribe
Login
Notify of
guest

guest

0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments

Recent Comments

  1. Lillie on MASWALI YA KITABU CHA 1 WAFALME, I
  2. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI, INJILI YA MATHAYO
  3. Noel Swai on MASWALI, INJILI YA MATHAYO
  4. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI YA KITABU CHA YOSHUA I
  5. watakatifuwasikuzamwisho on MASWALI YA KITABU CHA MWANZO

Palipo na Roho wa Bwana hapo ndipo penye uhuru
©2025 NDOTO ZANGU | Powered by SuperbThemes & WordPress
wpDiscuz